Biashara Yavuma Mjini Rongai

Esther Okumu                                                                                                 18/7/2016

Mavazi ni mojawapo ya mahitaji muhimu ya binadamu, wanabiashara haswa wale wanaouza nguo kama kofia, fulana na soksi mjini Rongai, wanasema kuwa msimu huu wa mvua na baridi umewaletea mapato mazuri.

Ingawa wanabiashara wengine kama wale wanaouza bidhaa kama nyanya wanalalamika kuwa msimu huu wa mvua na baridi umewaletea hasara, wale wanaouza nguo haswa zile za mitumba wanapata faida kubwa sana. Mwanabiashara mmoja mjini Rongai alisema kuwa biashara wanayofanya inawapa pesa nzuri na hawaoni tatizo lolote . Kwa sasa ni biashara ya mitumba inayovuma na kwa hakika wanabiashara hao wa nguo wanapata mapato mazuri.

###

This entry was posted in NEWS and tagged , , . Bookmark the permalink.

Leave a comment